26 Januari 2015

MAHITAJI MUHIMU KWA KIDATO CHA MAANDALIZI - 2015

Mwanao anapaswa kuripoti shuleni siku ya Jumamosi, tar. 7 Februari 2015 saa 3 asubuhi.

KARO:
  1. Mang'ola -- sh. 300,000/- kwa mwaka
  2. Nje ya Mang'ola -- sh. 400,000/- kwa mwaka
NB: KARO INAWEZA KULIPWA KWA AWAMU.
Karo ilipwe kupitia moja ya akaunti zifuatazo:
  • Exim Bank – Karatu A/C No. 0120005247 Anna Gamazo SS
  • NBC Bank – Karatu A/C No. 045201010908 Anna Gamazo SS
MICHANGO

Sh. 165,000/- fedha hii kwa ajili ya sare na michango ya uendeshaji. Inalipwa yote siku ya kujiunga.

MAHITAJI:
  1. Mwanafunzi anapaswa kujinunulia sweta jeusi (sio koti na isiwe na kofia) kwa ajili ya kutumia baada ya masomo.
  2. Raba nyeupe (isiyokuwa na mchanganyiko wa rangi) kwa ajili ya michezo.
  3. Jozi za kutosha za soksi nyeupe ndefu zinazofika chini ya goti
  4. Viatu vyeusi vya ngozi (leather shoes) vyenye kufungwa kwa kamba, jozi mbili.
  5. Shumizi na sidiria nyeupe au fulana nyeupe kwa ajili ya kuvaa ndani ya shati.
  6. Vipodozi vyovyote (losheni, glycerine, poda, marashi) haviruhusiwi. Aje na mafuta ya mgando (petroleum jelly) pekee
VIFAA VYA KAZI:
  • ndoo mbili kwa ajili ya kuogea na kuchotea maji, 
  • jembe lenye mpini
  • ufagio wa chelewa, na
  • ream moja ya karatasi zenye mistari (ikabidhiwe kwa mhasibu siku ya kuripoti)
VIFAA VYA DARASANI:
  1. Mathematical set (mkebe wa Hisabati)
  2. Madaftari angalau 10 (inashauriwa kununua counter books angalau zenye quire 2)
  3. Vifaa vya kuandikia kama vile kalamu, penseli, crayons na rula
  4. Kamusi ya Kiingereza (unashauriwa kununua “Oxford Basic Engish Dictionary (3rd au 4th ed.)” au “Oxford Student’s Dictionary”) Kamusi za English-Kiswahili hazishauriwi
VIFAA VYA BWENINI:
  • Godoro lenye mfuniko la futi 2.5 kwa 6
  • Chandarua ya mbu (ya mviringo) ya rangi ya blue pekee
  • Taulo moja (rangi yeyote) kubwa na nguo ya usiku moja (night dress)
  • Sabuni za kufulia na kuogea za kutosha, mswaki na dawa ya meno na tochi ya kurunzi (tochi ya kuchaji hairuhusiwi). Taa za sola ni bora zaidi.
  • Kitenge au kanga kwa ajili ya kujifunga wakati wa kwenda kuoga.
  • Sanduku kubwa (tranka) pamoja na mfuko wa safari (begi)

0 maoni:

Chapisha Maoni